TIC kuimarisha mifumo ya uwekezaji Nchini

Na Beatrice Sanga, MAELEZO. Kituo cha Uwekezaji Tanzania-TIC kimeanza kufanya maboresho ya huduma za uwekezaji kwa kuunganisha mifumo ya kielektroniki kwataasisi na idara 11 za Serikali zinazotoa huduma za mfumo wa mahala pamoja lengo likiwa ni kurahisisha utoaji wa vibali na leseni zauwekezaji kwa kuunganisha mifumo hiyo ili kuwa na dirisha moja la uwekezaji nchini